Baba mzazi wa Akwelina awaomba kitu Watanzania, Waziri Ndalichako atangaza neema
Safari ya mwisho ya mwili wa mwanafunzi, Akwelina Akwilini aliyepigwa risasi Februari 16, 2018 hatimaye imefika mwisho leo Ijumaa ya Februari 23, 2018 kwa kuzikwa huko Rombo mkoani Kilimanjaro.
Wazazi wa Akwelina wakiweka mashada kwenye kaburi la mtoto wao
“Binti huyu ambaye tumempumzisha kwenye nyumba yake ya milele alikuwa anapambana katika kusaka elimu ili aweze kuikwamua familia yake nimesikitika pia kuona kwamba pamoja na fedha zile ambazo Akwelina alikuwa anapata kwa ajili ya yeye kujikimu lakini alikuwa anatumia fedha hizo hizo kumsaidia mdogo wake Angela ambaye yupo kidato cha tatu naomba nisema kwamba huyo binti Angela nitamchukua kwa sababu natambua na kuthamini elimu hivyo nitahakikisha kwamba namsomesha mpaka uwezo wake na ndoto zake zitakapofikia,”amesema Prof. Ndalichako wakati wa kuuaga mwili wa Akwelina.
Waziri Ndalichako akitoa pole kwa wazazi wa Akwelina
Hata hivyo mama Mzanzi wa Marehemu Akwilina alipohojiwa na Bongo5 ameshindwa kuongea huku machozi yakimtoka kwa uchungu wa mwanaye.
No comments