Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Mhe. Zitto Kabwe ameachiwa na
Polisi kwa dhamana yenye thamani ya Tsh milioni 50 asubuhi hii mjini
Morogoro baada ya kulala mahabusu tangu jana Alhamisi Februari 22, 2018
usiku.

Zitto Kabwe
Taarifa hizo zimethibitishwa na Wakili wa Mbunge huyo wa Kigoma
Mjini, Ndg Emmanuel Mvula ambaye ndiye aliyemdhamini Zitto Kabwe na
kusema kuwa anatakiwa kuripoti katika kituo kikuu cha Polisi cha Mkoa wa
Morogoro siku ya Jumatatu Machi 12, 2018.
Mhe. Zitto Kabwe alikamatwa jana Februari 22, 2018 na Jeshi la Polisi
Mkoani Morogoro wakati akiwa katika ziara ya Chama cha ACT Wazalendo
inayoendelea kufanywa na chama hicho katika mikoa 8 Tanzania bara.
No comments