Header Ads

Yatima zaidi ya 200 wakumbukwa Dar


Taasisi ya Abdulah Aid, Markaz Kiwalani ya jijini Dar es Salaam imetoa msaada wa Mabegi na vifaa vya shule kwa watoto yatima 200 kutoka vituo mbalimbali  vya kulelea watoto hao jijini Dar es Salaam.

 Akipokea Msaada huo kwaniaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Diwani wa Kata ya Vingunguti ambaye pia ni Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala Omary Kumbilamoto ameishukuru taasisi hiyo na kuitaka taasisi nyingine kuiga mfano wa Taasisi hiyo ili kuungana mkono juhudi za serikali ya awamu ya tano katika kutoa elimu bure kwa watoto wa Tanzania.


Aidha kuelekea kusherehekea sikukuu ya EID-EL-FITRI Taasisi hiyo imegawa mafuta gallon 200 za Lita moja moja kuku 200  na Mchele  mifuko 200 ya kila  na nusu.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Taasisi ya Abdulah Aid sheik Arif Abdlahaman, amesema ametoa vifaa hivyo ili viweze kuwa saidia watoto hao na wao waweze kula sikukuu kwa amani.




No comments

Powered by Blogger.