CHADEMA Walia Rafu Tena....Ni Baada ya Mgombea Wao Kuengeuliwa na wa CCM Kupita Bila Kupingwa Korogwe Vijijini
Mgombea wa ubunge Korogwe Vijijini (CCM), Timotheo Mzava amepita bila kupingwa katika uchaguzi wa mdogo wa marudio.
Hatua hiyo imekuja baada ya Mzava kujikuta pekee yake muda wa kurudisha fomu ambao mwisho ulikuwa jana Agosti 20, 2018.
Mkurugenzi Mtendaji wa Korogwe, Dk George Nyaronga ambaye ndio msimamizi wa uchaguzi katika jimbo hilo amesema, “mgombea wa CCM amepita bila kupingwa.”
Awali Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa, alilalamika 'rafu' iliyochezwa baada ya mgombea wake katika jimbo hilo kuenguliwa kwa kushindwa kurejesha fomu kwa msimamizi wa uchaguzi huo.
Golugwa, amesema alifika katika ofisi ya msimamizi wa uchaguzi huo akiwa na mgombe wao, Amani Saguti majira ya saa 5:38 asubuhi kwa lengo la kurudisha fomu.
Amedai kuwa walipofika katika ofisi hiyo, walimkuta msimamizi wa uchaguzi, Samia Guram, lakini alikataa kuzipokea fomu hizo kwa madai kuwa muda wa kurudisha fomu ulikuwa haujafika.
Jimbo la Korogwe Vijijini limekuwa wazi kufuatia kifo cha aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Stephen Ngonyani maarufu kama Maji Marefu.

No comments