Header Ads

FEDHEHA 10 AMBAZO MASHABIKI WA UNITED HAWATAKUJA KUZISAHAU.


Usiku wa December 20, 2017 ulikuwa aibu na majonzi kwa mashabiki wa United baada ya timu yao kutolewa katika michuano ya Carbao Cup, wengi wanajipa moyo kuwa hawakulihitaji kombe hilo ila kiuhalisia roho zinawauma, tuone matokeo 10 yaliyowahi kuwaumiza United.

10.Manchester United vs Southampton 1976. Hii ilikuwa fainali ya michuano ya FA, Southampton hawakupewa nafasi hata kidogo kwani hata maandalizi yao yalikuwa ya hovyo, lakini siku ya mechi bao pekee la Bobby Stokes liliizamisha United.
09.Mk Dons vs Manchester United 2014.Hii inakumbukwa sana na mashabiki wa United ilikuwa August 26, moja ya vitu United walitamani kuviona ni mchezaji wao mpya Angel Di Maria, Mk Dons ambayo ilitengenezwa na wachezaji wengi wa chuo waliiadhiri United kwa kuipiga bao 4 kwa nunge.
08.Manchester United vs Leeds 2010.Ilikuwa raundi ya 3 ya michuano ya FA na atakayepigwa anaondoka, siku ya January 4 hakuna shabiki wa United aliyekuwa na hofu na vibonde Leeds kwa kuwa walikuwa wakienda Old Traford lakini United walishangazwa na bao la Jermaine Beckford lililoilaza United.
07.Bournemouth vs Manchester United 1982.United walipigwa bao 2 ugenini huku wakati huo kocha Harry Reknapp ndio alikuwa akianza anza ukocha akiwa anaifundisha Bournemouth na baada ya Reknapp kuiua United alikiri kwamba hiyo ndio ilikuwa siku ya furaha kubwa maishani mwake.
06.Manchester United vs York 1995.David Beckham alikuwepo, Phill Neville alikuwepo na Paul Scholes alikuwepo na walikuwa Old Traford lakini bado walishangazwa na timu kutoka daraja la pili York ambao waliichapa United kwa mabao 3 kwa nunge.
05.Southend vs Manchester United 2006. November 7 mwaka 2006 katika raundi ya nne ya FA, United waliwafuata Southend wanaoonekana ni vibonde, bao la Southend liliwapa furaha kubwa mashabiki wao kiasi cha kufanya wachezaji wa United kutolewa uwanjani chini ya ulinzi wa polisi baada ya mashabiki wa Southend kuvamia uwanja.
04.Manchester United vs Norwich 1967. Hii ilikuwa mwezi February katika raundi ya 4 ya FA, majina makubwa akiwemo Sir Bobby Charlton yalitosha kutabiri kwamba Norwich wanakwenda kuchezea kichapo lakini mchezo ukaisha kwa Norwich kuibuka kidede kwa mabao 2 kwa 1.
03.Manchester vs Middlesbrough 2015. Hii ilikuwa sare ya bila kufungana katika uwanja wa Old Traford, lakini suluhu hii ilishuhudia United wakiondolewa katika kombe la ligi kwani tayari mchezo wa kwanza walitoka kupigwa mabao 3 kwa 1.
02.Manchester United vs Crystal Palace 2011. Robo fainali ya kombe la ligi mwezi November 2011, Old Traford palionekana panaweza kuwa mwisho wa Crystal Palace kutokana na nguvu waliyokuwa nayo United lakini bao la dakika za nyongeza la Glen Murray liliufanya mchezo huo kuisha kwa Palace kuibuka kidedea kwa bao 2 kwa 1.

01.Bristol vs Manchester United 2017. Hii ndio habari kubwa wiki hii , ambapo mashabiki wa Manchester United hawakuamini baada ya safari yao ya EFL Cup kukatishwa na timu ambayo haipo hata ligi kuu kwa mabao 2 kwa 1.

No comments

Powered by Blogger.