Polisi wanane wauawa baada ya kulipukiwa na bomu nchini Kenya
Askari Polisi waripotiwa kuuawa baada ya kulipukiwa na bomu la kutegwa ardhi katika kaunti ya Wajir nchini Kenya. Kiongozi wa eneo la Kaskazini-Mashariki mwa Kenya Muhammad Saleh amefahamisha kuwa wahalifu waliotega bomu hilo walishambuliwa baada ya kubainika kuhusika na tukio hilo.
Tukio hilo limetokea siku chache baada ya walinda usalama 6 kuuawa Liboi Garissa mpakani mwa Kenya na Somalia.
Kundi la wanamgambo wa al shabaab wanashukiwa kuhusika na ktendo hicho. Mashambulizi kama hayo nchini Kenya yanalenga jeshi la Kenya linalochunga usalama katika eneo hilo

No comments